Wednesday, May 30, 2012

Wema Sepetu Avishwa Pete ya Uchumba na Mwinyi wa Machozi Band-Soma Ziadi Hapo chini Upate kweli

 Mwigizaji Wema Sepetu bado anaendelea kuishoot movie yake ya kwanza iitwayo SUPER STAR ambayo inahusiana na maisha yake kwa asilimia kubwa sana, ikiwa ni movie ambayo itaonyesha vitu vingi alivyovipitia kwenye umaarufu wake. Usiku wa May 29 kuamkia may 30 2012 saa nane na dakika kumi ndani ya Maisha Club Dar es salaam, Wema alivishwa pete na mwimbaji Mwinyi wa Machozi Band ambae kwenye hiyo movie yeye atazicheza nafasi zote za Mwimbaji Diamond Platnums aliyewahi kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu, Mwinyi amecheza kama Diamond ambae pia alimvisha Wema pete ya uchumba hapohapo Maisha Club. Akiongea Exclusive na millardayo.com Wema amesema bajeti ya kutengeneza hiyo movie ni kuanzia milioni 29 mpaka 30 ambapo alianza kuitengeneza march mwaka huu na ataizindua june 23 2012. Mrembo huyu ambae ni Miss Tanzania 2006 amesema mwanzoni alikua anataka hii movie wacheze Irene Uwoya na Jb na ilikua haikua ikihusu maisha ya Wema lakini baada ya Jb kuwa na kazi nyingi, alifikiria kucheza movie mwenyewe na kupewa idea ya Super Star na msanii Suma Lee. Alichofanya baada ya kupewa hiyo idea na Suma Lee ni kuipimp na kuongeza matukio mengi aliyokutana nayo kwenye umaarufu na ni movie ambayo mastaa wengi wa kibongo wameuza sura ndani yake.




No comments:

Post a Comment