Thursday, May 31, 2012

Anti Ezekieli: Beef Langu na Ray, Steve Limekwisha



BIFU la muda mrefu lililokuwepo kati ya wasanii wa filamu, Aunt Ezekiel, Steven Mangere ‘Nyerere’ na Vincent Kigosi ‘Ray’ limezimika baada ya mastaa hao kukaa na kuamua kumaliza tofauti zao.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni katika Pub yake iliyopo Mwananyamala jijini Dar, Aunt alisema bifu hilo lililowafanya kutoshirikiana katika mambo ya kimaendeleo kwa muda mrefu lilikuwa likiwaathiri sana hivyo wakaamua kukubali yaishe.
“Unajua kifo cha Kanumba ndicho kilichotufanya sisi waigizaji tuwe kitu kimoja na kumaliza tofauti zetu ndiyo maana unamuona Ray na Steve wako hapa kwenye Pub yangu kuonyesha ni jinsi gani tunaungana mkono katika masuala ya maendeleo na si kuwekeana chuki zisizo na maana,” alisema Aunt.

No comments:

Post a Comment